Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk, Hussein Ali Mwinyi ameiagiza Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kuhakikisha Wanafunzi wote wenye sifa za kupatiwa mikopo ya Elimu ya juu wanapatiwa mikopo hio ili kuendelea na Elimu ya juu kwa wakati.Rais Dk ,Mwinyi ambae ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Zanzibar SUZA ametoa tamko hilo alipowatunuku Vyeti Wahitimu wa Ngazi mbalimbali katika Mahafali ya 20 ya Chuo hicho yaliofanyika Ukumbi wa Dk, Ali Mohamed Shein Tunguu, Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja.
Dk,Mwinyi ameeleza kuwa kwa kutambua Umuhimu wa Elimu Serikali itaendelea kuchukua kila juhudi kuhakikisha mazingira Bora ya Upatikanaji wa Elimu kwa ngazi zote ili kuwa na wana taaluma wenye weledi ,ujuzi utakaochochea maendeleo na Ukuaji wa Uchumi.Rais Dk , Mwinyi ameeleza kufarijika na ongezeko la Wahitimu wa Chuo hicho kila mwaka hatua inayoakisi dhamira ya Chuo hicho ya kuwa chachu ya Maendeleo ya Kiuchumi kupitia Chuo hicho.
Rais Dk, Mwinyi ambae ni Mkuu wa Chuo hicho ameeleza kufarijika na ongezeko la asilimia 8.4 la Wahitimu mwaka 2023-2024 ongezeko la wahitimu 2,291 ukilinganisha na wahitimu 2,101 mwaka uliopita pamoja na ongezeko la Wahitimu Wanawake kwa asilimia 61 na kuwataka kuwa sehemu ya mabadiliko chanya kwenye Maendeleo ya jamii.Rais Dk, Mwinyi amefahamisha kuwa Serikali imetenga kiasi cha shillingi Billion 33.4 kwa ajili ya mikopo na Wanafunzi 8.870 wanatarajiwa kupatiwa mikopo hiyo.
Aidha ameeleza kuwa Serikali itaendelea kuandaa programu mbali mbali katika Taasisi za Kitaaluma za ndani ya nchi na kimataifa ili kuinua kiwango cha Taaluma kwa Wataalamu ,Wafanyakazi na Wahadhiri wa Suza ili kuongeza hadhi ya Chuo na kuwa Chenye kutoa Elimu bora.Amesisitiza kuwa lengo ni kuwa na Chuo kinachotoa Wahitimu wenye sifa ,weledi na ujuzi watakaoweza kuhimili Ushindani katika soko la ajira , au kujiajiri wenyewe na kuendana na kasi ya Maendeleo iliopo hivi sasa
Amebainisha kuwa Serikali imejikita katika kuimarisha Ubora wa Elimu kwa kutoa Mafunzo Endelevu kwa Wahadhiri na Watumishi Waendeshaji wa Suza kwa kushirikiana na Taasisi za Kimataifa ili kuleta programu Bora na zinazokidhi viwango vya Kimatiafa. Amelipongeza Baraza la Chuo hicho kwa kufundisha Shahada ya Sayansi ya Utabibu ya Kinywa na Meno na kuanzisha programu nyengine mpya nne za Elimu Chuoni hapo ikiwemo Shahada ya Elimu Mjumishi na mahitaji maalum ya Kielimu,Shahada ya Elimu ya Amali na Shahada ya Elimu na lugha pamoja Shahada ya Mafunzo ya Ubaharia inayotarajiwa kuanza kufundishwa mwaka 2025.
Rais Dk, Mwinyi amesema hatua hiyo itaiwezesha Serikali kuwa na Wataalamu wa kutosha katika sekta mbalimbali watakaotoa mchango wao katika Maendeleo ya kijamii.Aidha Rais Dk, Mwinyi alimtunuku Waziri wa Nchì ,Afisi ya Rais ,Katiba Sheria ,Utumishi na Utawala Bora Haroun Ali Suleiman Shahada ya Uzamivu ya Heshima ya Elimu ya Chuo Kikuu cha Zanzibar SUZA.
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Lela Moh’d Mussa ameeleza kuwa Chuo hicho kimekuwa Alama Maalum ya Utambulisho wa Zanzibar Kitaaluma kwa mafanikio ya kutoa wahitimu na taaluma Bora.Ameielezea fursa ya kuwepo kwa mikopo kwa Wanafunzi wa ngazi ya Diploma kumeongeza Idadi ya Wanafunzi Wanafunzi wamejiunga na Chuo hicho kwa ngazi hiyo na kuahidi kwa Wizara hiyo kuhakikisha Chuo Kinaimarika na kupata hadhi kimataifa.
Makamu Mkuu wa SUZA Prof, Makame Haji ameielezea mipango Bora ya Serikali ya Awamu ya Nane na Miongozo ,Busara na Hekima Za Rais Dk, Mwinyi zimekuwa kichocheo cha mabadiliko na Maendeleo makubwa ya Chuo hicho.Amfahamisha kuwa kufuatia Ongezeko la Wahitimu Chuo kina Mpango kuendesha Miradi tofauti ya Upanuzi wa Miundombinuya majengo ya Chuo hicho kwa kuwa na majengo ya ghorofa kupitia Mpango Mkuu wa Chuo hicho.
Hatua hiyo itaambatana na Ujenzi wa Maabara ya Sayansi ,Skuli ya Kilimo ,Skuli ya Elimu ya Lugha za Kigeni ,Ujenzi wa Skuli ya Afya ,Sayansi na Tiba ikiwa miongoni mwa Miradi zaidi ya Wahitimu 2,200.wa ngazi ya Vyeti,stashahada, Shahada, na Shahada ya Uzamili na Uzamivu wametunukiwa Vyeti vyao katika Mahafali hayo.